Posts

Showing posts from October, 2020

Neno La Ushindi__04; Nyenyekea chini ya Mkono wa Mungu, ili akukweze na kukuinua kwa wakati wake.

Image
 Neno La Ushindi__04; Nyenyekea chini ya Mkono wa Mungu, ili akukweze na kukuinua kwa wakati wake. 1 Petro 5:6-7 " Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu. Kila mmoja  wetu anataka kufika mbali_mafanikio makubwa sana katika maisha yetu. Pengine kwenye huduma , kazinj kwako na maeneo mbalimbali ya maisha yako. Ipo kanuni moja hapa ambayo tunakwenda kujifunza kwa upana wake, na nina Imani inakwenda kukusaidia kwa viwango vikubwa sana. Kanuni hiyo ni KUNYENYEKEA.Maandiko matakatifu yanaeleza kuhusiana na unyenyekevu, Ya kwamba ili mtu aweze  Kuinuliwa na Mungu, Kupanda viwango vya huduma ni lazima anyenyekee. Maana Ya unyenyekevu ni kujishusha na kuona si kitu na  kumwinua Mungu zaidi na kumpa nafasi ya kwamba anaweza kufanya mambo makubwa. Unaponyenyekea unakuwa na Maana ya kwamba wewe sio kitu na peke yao hauwezi kufanya chochote.....

Neno La Ushindi___01; Mweleze Mungu shida zako, naye atafanya Mlango nawe utamtukuza.

Image
  Neno La Ushindi___01; Mweleze Mungu shida zako, naye atafanya Mlango nawe utamtukuza. Zaburi 50:15 " Ukaniite siku ya Mateso, Nitakuokoa na wewe utanitukuza. Huu ni wito wa Mungu kwetu pale tunapokuwa tunapitia katika shida, mateso mbalimbali. Ya kwamba tumuite Yeye (Mungu ) naye atatusikia na kutuokoa_Uponyaji, kufunguliwa amani, furaha n.k. Mara nyingi tumekuwa tunawaza na kuwazua wakati pale Magumu yanapotukia katika maisha yetu.Tunaanza kuyafikiria sisi kwanza, badala ya Kuyapeleka kwa Mungu kwanza. Hivi ndiyo njia sahihi ya kuyapokea matatizo katika maisha yetu.TUMUITE BWANA YESU KATIKA MATESO YETU.na Mungu anakwenda kutuokoa Haijalishi ni mambo makubwa kiasi gani yanayokusumbua , Lakini hili ndiyo ahadi ya Mungu. 1.Hakuna Ambalo Kwa Mungu haliwezekani_ Mambo yote kwake yanawezekana. Luka 1:37 " kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu" Yeremi 32:27 "Tazama, mimi ni BWANA, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lolote nisiloliweza?" 2.Omba lo...