YOU SHOULD UNDERSTAND THIS PLEASE

(UNATAKIWA KUELEWA NA KUFAHAMU HILI).

                                       


Church is hospital, that's why it's not everybody you meet in church you can marry.

Kanisani ni hospitali, na ndo maana si kila mtu unayekutana naye, unaweza kumuoa/kuolewa naye
Church is hospital and good hospital is known by the amount of sick people you see in it.
Kanisa ni hospital na hospital nzuri inajulikana au inatambulika kwa idadi ya wagonjwa unaowaona katika hospitali hiyo.

Huwezi kusema hospitali fulani ni nzuri na ya Kimataifa halafu ndani yake hamna mgonjwa hata mmoja.
Unapoenda hospital na kukutana wagonjwa wengi, mwingine anasumbuliwa na mguu, mwingine unamwona anaharisha pale, mwingine anatapika pale, mwingine yuko mahututi n.k hiyo ni ISHARA ya Kuonyesha kuwa ni Hospital nzuri na wanafanya kazi.

Kwa maana hiyo hospital nzuri ni ile ambayo ina wagonjwa wengi ambao wanashughulikiwa.
Na KANISA ZURI NI KAMA HOSPITAL NZURI,

Kanisani tuna WAONGO, WALEVI, WAZINZI , wako wenye hasira kali, ni hilo ndilo KANISA ZURI wako hapo KUHUDUMIWA MAGONJWA yao na shida mbalimbali walizo nazo.
Wako ambao WANAKUBALI KUHUDUMIWA na kuna ambao HAWAKO TAYARI KUHUDUMIWA.
Kwa hiyo si kila unayekutana naye KANISANI, anafaa kuwa MUME WAKO/MKE WAKO.

(In church we have insane people, we have fraudsters, we have liars, and cheats, we have angry people, that's is good Church .We are giving them treatment, some are responding while others are not yet responding.So It's not everyone you meet in church you can marry).

NINI FUNZO HAPA(TUNAJIFUNZA NINI).
Usidanganyike kwamba kila mtu anayekutana naye [Kanisani] ukadhani ni mtu sahihi kwako. Wengine wako hapo kwa sababu fulani fulani.
Usianzishe tu mahusiano na dada/kaka aliyeko kanisani(kwa sababu yuko kanisani) kabla ya kumfahamu vyema kwa undani wake.Nenda kwa Mchungaji wake akwambie kiundani, unaweza ukawaza kuanzisha Mahusiano kumbe ameshachumbiwa au kuolewa kabisa.
Jifunze kupokea Ushauri kabla ya kuanzisha mahusiano yoyote yale.....
Joshua Golyama
+255 764 257 495 (Whatsapp)
Inspired by Kingslev Okonkwo The Author of Book Who Should I marry.


Comments

Popular posts from this blog

Neno La Ushindi___01; Mweleze Mungu shida zako, naye atafanya Mlango nawe utamtukuza.

USIKATE TAMAA.....

NAMNA YA KUANZA UPYA