GHARAMA YA KUJILINGANISHA NA WENGINE

 GHARAMA YA KUJILINGANISHA NA WENGINE

 
Don't compare yourself with someone else!!!

....unapoteza kusudi lako
 
....Unapoteza upekee wako
 
....Unapoteza uwezo wako
 
....Hautafanya kwa viwango ulivyotakiwa.
 
....Hautakuwa na matokeo makubwa
 
....Huwezi kuwa mkuu kwenye eneo lako kwa kuwa photocopy ya mtu mwingine
 
.....Unapoteza rasilimali zilizoandaliwa kutimiza kusudi lako.
 
...God's provisions, alizoandaa Mungu kwa ajili yako..God will never fund something else out of his purpose
 
Mungu huwa hatoi rasilimali bure..huwa anatoa rasilimali kwa ajili ya kukamilisha kusudi lake.
 
Unaweza kujifunza kwa wengine wanaofanya vizuri ili uwe bora 
 
Huwezi kuwa bora kwa kuiga bali kwa kujifunza...
 
Kila mtu anao upekee wake unaomfanya yeye awe bora 
 
Ndani yako Kuna upekee wako wa kukufanya bora...kwa kujifunza unaendelea kuchonga ubora unaoutaka.
 
Jipime wewe kama wewe,jipime wewe kama unafanya inavyotakiwa ..usijipime kwa kujilinganisha na watu.
 
Jilinganishe wewe ulivyo na wewe unayepaswa kuwa usijilinganishe na watu umeumbwa kwa utofauti na upekee wako,umebeba kusudi tofauti,utendaji wako uko tofauti na wengine..ukianza kujilinganisha unapoteza upekee wako.
 
Hupaswi kujilinganisha na mtu yeyote kwa sababu huyo anayo assignment tofauti na yako,anao upekee wake, amepewa kufanya kazi kwa utofauti na wewe.
 
2 Kor 10:12-18
Huyu ni Petro anaeleza vile anavyojipima yeye kama yeye bila kujilinganisha na wengine usijisifu kwa vipimo vingine..jipime kwenye kusudi lako ulilopewa kutimiza. usijipime kwa vipimo vya watu wengine...
 
Kila mtu kapewa assignment yake aikamilishe
usijipime utendaji wako na utendaji wa mtu mwingine,usijipime zaidi ya vile unavyotakiwa wewe...
 
Kuna mahali Mungu anakutaka wewe ufike,usijipimie kuwa umefika kwa sababu Kuna watu bado hawajafika mahali ulipo wewe au usijipimie kwamba bado hujafikia kwa sababu kuna watu wamekutangulia sana.
 
Tunajipima sisi na matokeo yale tuliyopaswa kuwa nayo na sio sisi na matokeo ya wengine.
 
Alphoncina Clement
 
0714607811
 
Divine Restoration
 
The Essence of Purpose Discovery

Comments

Popular posts from this blog

Neno La Ushindi___01; Mweleze Mungu shida zako, naye atafanya Mlango nawe utamtukuza.

USIKATE TAMAA.....

Neno La Ushindi__04; Nyenyekea chini ya Mkono wa Mungu, ili akukweze na kukuinua kwa wakati wake.